Sunday, 24 March 2019

Kua wa kwanza kurudisha tabasam la mtoto yatim, tabasam ambalo aliweza kulipoteza kwa kuondokewa na wazazi wake. hali ya kua aliamini kwamba wangeweza kumlea bila wasiwasi wowote wala mashaka yeyote, lakini ndoto zake zili potea gizani punde tu alipo kua pekeake na kujikuta ana kosa haki zake za msingi kwa ndugu jamaa na marafiki, ewe muungwana ungana nasi katika kuwalea watoto hawa kwa kuwapatia mambo mbalimbali ili nao waje kua watoto bora na mahiri ilimradi na wao pia waje kuwasaidia wenzao badae.  #wanandoto  shukra za dhati ziwaendee ndugu zetu walioko ufaransa wazazi wa Airon kwani mchango wenu ume weza tufanye mabadiriko tuna washukuru sana

Sunday, 10 March 2019

Al-zam orphanage Center our Motto Mkombozi na tabasam la mtoto yatima






Hivi ni baadhi ya Vitanda wanavyo lalia Watoto ila vipo vichache kwani wengine ikifika usiku wana lala chini hivyo ewe mdau ambae uta guswa na suala hili tafadhali tuna hitaji mssada wa nagodoro na Vitanda 25 Double deka ili hawa wengine wanao lala chini wafarijike.

 kituo hiki kipo maeneo ya Mbagala Kichemchem mtaa wa kwa Gobwa tuna washukuru sana na pia karibuni sana muda wowote saa yeyote. 

Saturday, 9 March 2019

Karibuni Al-zam Orphanage Center mkombozi na tabasam la watoto yatima


kama mnavy ona tuna kabiliwa na changamoto nyingi sana ikiwemo mahali pa kupikia,vitanda,magodoro,mavazi,makazi ya kudumu na mengine mengi hapa tunapo ishi ni nyumba ya kupanga kiasi ambacho ina tugharimu kulipia kila mwaka pesa talim 1,500,000 kwa mwaka kama unavyo jua kituo hiki hakina mfadhili wa kudumu hivyo tuna pitiaga wakati mgumu katika kulipia kodi ya ya pango pia Ada za shule,bili za maji na umeme na mengine mengi ewe mdau tuna omba support yako ili kuweza kuwalea watoto hawa katika mazingira mazuri na yenye amani










Wasanii ni kio cha jamii ama kwa hakika tume farijika sana kwa kuja kujumuika na watoto hawa kwani hapa tanzania kuna vituo vingi sana ili mmeweza kukaa na kujadiliana na kuona bora mje hapa hiyo ni heshima kwetu pia hata watoto wame furahi sann walikua wakiwaona tu kwenye tv hatimae wamewaona live pia tuna wapongeza sana sio kama mna uwezo hapana ila moyo wa huruma na upendo kwa watoto hawa tuna toa shukrani zetu za dhati kwa Riyama Ally na JB ninyi ndio mmekua mstari wa mbele katika kutusaidia pia tuna washukuru wote mlio hudhuria tuna sema tuna wapenda sana pia kwa wale wote pia karibuni sana hapa ni kama nyumbani kwenu na hawa ni watoto wenu msisite kufika










Friday, 24 August 2018

@alzam







hawa ni miongon mwa wanafunz wa chuo kikuu cha uhasibu (TIA) kilichopo uhasibu walikuja kujumuika na watoto tuna washukuru kwa kujitolea muda wenu na kuja jumuika na watoto hawa mungu atawalipa

Monday, 11 September 2017

Hayo matenga muyaonayo hapo ni matenga ya nyanya ila kutokana na ubunifu tulip weza kufanya ili kuhidhi nguo za watoto kuto kuzagaa hivyo basi  ime tulazimu kuyafanya makabati kiukweli bado tuna hitaji support zenu ili tuweze kuwalea watoto hawa katika malezi bora kwa jukumu ni letu sote #wanandoto